Njia 5 rahisi za kuanzisha biashara yako

Hamjambo wasichana. Jina langu ni Czarina na nilipokuwa na umri wa miaka 15, nilianzisha biashara yangu mwenyewe ya kuuza mapambo yaliyotengenezwa kwa mikono nje ya boma letu. Kila siku baada ya shule, ningeweka shanga pamoja na kubuni vipande vya kupendeza ambavyo baadaye ningevitengeza na kuviuza. Kwa sasa ninamiliki biashara yangu mwenyewe ya kutengeneza mapambo kwa ufanisi. Hizi hapa ni hatua zangu 5 za kuanzisha biashara ya kupendeza na kusimamia pesa zako!

1. Tafuta uchu wako na utengeneze MPANGO.

Hatua ya kwanza kwa mwanamke yeyote mfanyabiashara ni kutafuta uchu wake! Pengine una uchu kuhusu muziki au sanaa au huenda unapenda kufunza au spoti. Unapounganisha mpango wa biashara na uchu wako, utapata motisha zaidi ya kufanya kazi kwa bidii. Baada ya kuamua kuhusu kile unachokipenda, ni wakati wa kuandika MPANGO wako! Hatua hii itabadilisha ndoto yako kuwa lengo. Mpango wako wa biashara unapaswa kujumuisha:

  • Wazo lako la biashara
  • Soko lako unalolenga (wateja)
  • Malengo yako ya mauzo
  • Watakaowajibika katika kazi mbalimbali
  • Muda ambao mambo yanahitajika kufanywa

2. Tengeneza Bajeti!

Bajeti ni mpango wa vitendo vyako vya matumizi na bajeti ya kila mwezi inaweza kukusaidia kufanya hesabu kuhusu jinsi ya kutumia pesa zako kwa njia ya busara kila mwezi. Itahakikisha kuwa hutumii pesa zaidi na itayapa mahitaji yako kipaumbele dhidi ya vitu vya ziada. Andika mahitaji yako muhimu zaidi kwanza (chakula, makazi na matumizi ya biashara) na uone iwapo kuna gharama zozote ambazo unaweza kuziondoa (kama vile kununua chakula, huku ukiwa unaweza kutengeneza chakula chako ukiwa nyumbani.)

3. Anza kuweka Akiba!

Weka akiba ya kiasi kidogo cha pesa kila wiki. Hata sarafu chache zinaweza kuongeza hesabu na kukusaidia katika ndoto zako za biashara. Weka pesa zako mahali salama ambapo hamna mtu yeyote anayeweza kuzifikia. Katika hifadhi iliyofungwa au mahali pa siri ambapo ni wewe tu unayepajua.

Fanya kazi ndogo ndogo ili upate pesa za ziada. Kutunza watoto, kufunza au kupika yote ni mawazo bora zaidi.

Tengeneza bajeti ya kila mwezi. Andika matumizi na mapato yako yote ya kila mwezi. Rekodi hii itakusaidia kuweka akiba na kukuonyesha matumizi yako ya pesa.

4. Kufanya kazi huzuia mawazo ya mfanyabiashara.

Hatua ya kuchukua muda wako fulani kukaa na mfanyabiashara unayempenda inaweza kukusaidia kuwa mfanyabiashara bora. Wanaweza kukupa ushauri wa kweli na kushiriki mafanikio na upungufu wao pamoja nawe. Watakuwa pia na ushauri bora zaidi kuhusu jinsi ya kutengeneza bajeti na kuweka akiba na jinsi ya kutengeneza mpango wa biashara wa kupendeza.

5. JIAMINI!

Jambo la maana zaidi iwapo unataka kuanzisha biashara yenye ufanisi ni kujiamini! Wewe ni mtu wa kipekee na mawazo yako ni muhimu. Amini uwezo wako, fanya kazi kwa bidii na uweke akiba kwa njia bora. Mwangaza wako utang’aa zaidi na utakuwa mwanamke msimamizi wa kupendeza ambaye unatakiwa kuwa!

Share your feedback