Unahitaji motisha kuzungumza?

Nukuu hizi 7 zitakuwezesha kuzungumza

Ikiwa huzungumzi dunia itajuaje kuwa wewe upo? Wasichana, ulichonacho cha kusema kina maana! Jinsi unavyohisi kuhusu jambo fulani kuna maana kubwa. Unachofanya na sauti yako pia ni muhimu. Hapa kuna baadhi ya nukuu za kukuhamasisha kuzungumza na kusimamia mambo muhimu kwako!

"Usipozungumza watafikiri kuwa UKO SAWA jinsi mambo yanavyoendelea. Kimya huchukuliwa kama hali ya kukubali. "- Sanya Parker

"Watu wengi wanaogopa kusema wanachotaka. Ndiyo sababu hawapati wanachotaka. "- Madonna

"Usipozungumza hakuna kitakachobadilika. Kwa hivyo fanya mabadiliko, ili mradi ulijaribu ... unajua ulifanya KITU badala ya kukaa kimya. "- Haijulikani

"Umaskini unawezekana katika kila jamii kwa sababu mtu alikataa kuzungumza." - Sunday Adelaja

"Kila wakati msichana anapojisimamia mwenyewe, anasimama kwa ajili ya wasichana wote." - Maya Angelou

"Ikiwa unahisi kwamba kuna jambo mbaya, usiogope kuzungumza. Hata kama hudhani watasikiliza, sema tu. "- Haijulikani

"Dunia inakabiliwa mengi. Si kwa sababu ya watu waovu, bali kwa sababu ya ukimya wa watu wema. "- Haijulikani

Natumai umehamasishwa sasa ni wakati wa kuzungumza!

Share your feedback